Monday, January 17, 2011

usafi wa miji yetu

Usafi wa maisha yetu ni pamoja na mazingira tunayoishi kila siku.
Tuangalia tunapojenga majumba makubwa na marefu, je tuna vifaa vya kusafisha majengo hayo? Je matumizi yake yako sahihi, vilevile tuangalie kama kuna hatari yeyote inayoweza kutokea tutajikingaje?

Mfano mkubwa wa jengo kama hilo ni Jengo la Benjamini Mkapa Pension lililo pale Dar es salaam.
Jengo hili lina matumizi mbalimbali Lakini zile bakery na majiko yanaleta harufu ambayo sio nzuri. hasa pale supermarket.HATARI!!! je matumizi yake ni sawa? fume za kutoka jikoni zinaenda zimeelekezwa pa kwenda?

Lift za jengo hilo hazisafishwi, zinatumiwa na hoteli kubebea vyakula,takataka, Nguo chafu na maofisa kwa wakati huohuo. SHIDA!!!

Jamani usafi wa nje ya jengo unafanyika kwa kunin'ginia nje ya jengo hilo bila kinga yeyote.BALAA!

Kwanini Hoteli haitumii lift yake ambayo imeshatengwa kwa kazi hiyo?

Wadau wa mazingira na usalama mnasemaje?